John 12:1-6

Maria Ampaka Isa Mafuta Huko Bethania

(Mathayo 26:6-13; Marko 14:3-9)

1 aSiku sita kabla ya Pasaka, Isa alikwenda Bethania mahali ambako Lazaro aliyekuwa amefufuliwa na Isa alikuwa anaishi. 2 bWakaandaa karamu kwa heshima ya Isa. Martha akawahudumia wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Isa. 3 cKisha Maria akachukua chupa ya painti moja
Painti moja ni kama nusu lita.
yenye manukato ya nardo
Nardo ni aina ya mafuta yaliyokuwa yanatengenezwa kutokana na mimea yenye mizizi inayotoa harufu nzuri.
safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Isa na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.

4 fNdipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wale wanafunzi ambaye ndiye angemsaliti Isa, akasema, 5“Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari 300
Dinari 300 ni sawa na mshahara wa kibarua wa siku 300.
na fedha hizo wakapewa maskini?”
6 hYuda alisema hivi si kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi, kwani ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha akawa anaiba kile kilichowekwa humo.

Copyright information for SwhKC